~ INGEKUWA VIPI KAMA KILA PUMZI UNAYOIVUTA UNGEKUWA UNAILIPIA??~
Tuesday, October 09, 2007
Ama!! Tuiite nini? Dhihaka, kejeli, dharau, kutojua hesabu, kusoma au....

Tizama hiyo picha, tizama hiyo hundi anayokabidhiwa JK, tizama kiasi cha pesa kilichoandikwa katika hundi hiyo. Hebu kitizame tena kiasi kilichoandikwa kwenye hundi hiyo, kile kilichoandikwa kwa maneno, na kile kilichoandikwa kwa tarakimu. Ama!! Hivi "two hundred thousand" ni sawa na 300,000,= kweli? JK, hivi uliliona hilo lakini? sio changa la macho hilo? hapana, kuna walakini hapa!!


Picha hii ni kwa hisani ya mtandao wa gazeti la Majira, na maelezo ya picha hiyo katika gazeti la majira la leo, sanjari na kule kwenye mtandao nilipokutana nayo yalikuwa haya yafuatayo:-
RAIS Jakaya Kikwete akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Dola za Marekani 300,000 sawa na zaidi ya Shilingi za Tanzania Milioni 400 kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) kwa nchi ya Tanzania na Uganda Bw, John McIntire Dar es Salaam jana. (Picha na Rajabu Mhamila)
 
© Rama Msangi |Tarehe: 12:52 PM | Permalink |


Maoni: 2


  • Tarehe: October 9, 2007 at 1:18 PM, Mtoa Maoni:- Blogger Rashid Mkwinda

    araJamani hii ni aibu na hivi nadhani ndivyo tunavyodanganywa kila wakati, lakini hebu na tuangalie inawezekana jamaa kachukua cha juu akasahau kuweka vizuri tarakimu zake, utadhani ni mambo ya kusadikika kumbe ni vi2 halisi kabisa, jamani fedheha hii hadi lini? hadi Rais wetu anadanganywa ina maana....du nashindwa hata kusema...hiii coment nadhani hii ni coment ya mwaka binafsi nakupa tuzo kwani inaonekana ni wazi kuwa jicho lako la tatu linafanya kazi

     
  • Tarehe: October 25, 2007 at 7:10 PM, Mtoa Maoni:- Blogger kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa

    kwanza nikupongeze bwana rama. blog yako nimeipenda hasa kwa kuwa inaripot mambo ya mikoani. kwa maneno mengine ina ripot unrepoted world. congrats sana na tuko pamoja